.

.
.

.

.
.

.

.
.

.

.
.

.

.
.

.

.
.

.

.
.

Saturday, March 28, 2015

JK akamilisha uteuzi wa wabunge



Hatimaye Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Jakaya Mrisho Kikwete leo amekalisha uteuzi wa wabunge kwa mujibu wa ibara ya 66 kifungu (1) aya ya (e) ya  Katiba ya Jamhuri ya Muungano inayompa mamlaka ya kuteua watu wasiozidi kumi (10) kuwa Wabunge wa Bunge la Jamhuri ya Muungano. Katika uteuzi huu Rais amemteua Dkt. Grace Puja na Ndugu Innocent Sebba kuwa wabunge na tayari Spika wa Bunge la Tanzania Mhe. Anne Semamba Makinda (Mb) amewaapisha ili waweze kuanza kazi rasmi.

Wabunge walioteuliwa na Rais kwenye Bunge la Kumi kwa mujibu wa Katiba ni wafuatao:
1.     Mhe. Prof. Sospeter Mwijarubi Muhango
2.     Mhe. Dkt. Asha-Rose M. Migiro
3.     Mhe. Saada Mkuya Salum
4.     Mhe. James Francis Mbatia
5.     Mhe. Prof. Makame Mnyaa Mbarawa
6.     Mhe. Janet Zebedayo Mbene
7.     Mhe. Zakia Hamdani Meghji
8.     Mhe. Shamsi Vuai Nahodha
9.     Mhe Dkt. Grace Khwaya Puja na
10. Mhe. Innocent Rwabushaija Sebba

Kwa uteuzi huu idadi ya wabunge imetimia 357 kikatiba
Mteule Innocent Sebba akila kiapo cha utii

Spika Makinda akikabidhi vitendea kazi kwa Mbunge mteule Innocent Sebba. Anayeshuhudia ni Katibu wa Bunge Dkt. Thomas Kashillilah