.

.
.

.

.
.

.

.
.

.

.
.

.

.
.

.

.
.

.

.
.

Wednesday, May 20, 2015

Rais Filipe Jacinto Nyusi alihutubia Bunge

Viongozi wakimsubiri Rais wa Msumbiji 19 Mei 2015
Spika wa Bunge akimpokea mgeni wake, Rais wa Jamhuru ya Msumbiji Mhe. Filipe Jacinto Nyusi mjini Dodoma
Rais Nyus akipokea salamu rasmi



Rais Nyusi akikagua gwaride
Rais Nyusi akisaini kitabu cha wageni mashuhuri. Wanaoshudia ni Spika wa Bunge na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Jakaya Mrisho Kiwete


Rais wa Msimbiji akilihutubia Bunge la Jamhuri
Rais Kiwete akimsalimu na kumpa pole Mhe. Beatrice Shelukindo ambaye anaumwa



Spika Makinda akishauriana jambo na wakuu wa vyombo vya Dola

Picha ya pamoja


Tuesday, May 12, 2015

Politik in cross-road?


Picha nzima ilikuwa hivi ,

Mbunge Agustino Mrema alialikwa na kanisa la Kinjili La Kilutheli Tanzania KKKT dayosisi ya Kaskazini kwa ajili ya sherehe za kumbukumbu ya aliyekuwa askofu wa kwanza wa Kanisa hilo Stephano Moshi,mualiko ambao pia alipewa James Mbatia.

Wawili hawa bila kujua kama watakutana,Mrema ndiye aliwasili wa kwanza katika Usharika wa Kotela ambako zimefanyika sherehe hizo akiwa na gari lake na baadae aliwasili Mbatia ambaye yeye alikuwa na msafara wa magari mawili moja wapo likiwa limebeba wasaidizi wake ambalo lilikuwa na bendera kubwa ya chaa chake cha NCCR.

Moja kwa moja Mbatia alielekea katika eneo ambalo liliandaliwa kwa ajili ya kupta kifungua kinywa ambako tayari Mrema alikuwa amekwisha wasili na kila mmoja kuketi maeneo tofauti.

Wakati wakiendelea kupata kifungua kinywa ,ghafla liliwasili Coster ikiwa imepakwa rangi ya TLP na Bendera za chama hicho na kupaki ,hii nadhani wapambe wa mrema waliamua kufanya hivyo baada ya kuna tayari Mbatia kafika kanisani hapo huku gari lake likiwa na bendera kubwa.

Baada ya kupata chai waiwli hao walisaimiana na kuanza kuzungumzo bahati mbaya walizungumza kwa lugha ya nyumbani wote wawili hivyo ilikuwa ni vigumu kufahamu mara moja nini walikuwa wakizungumza.

·  Ibada ilianza na baadae Baba Askofu Dkt Fredrick Shookatika hotuba yake alionya wasaka uongozi kujipima kabla ya kuja kwa wananchi kuwaomba ridhaa huku akitaka waeleze nini wamefanya katika kuleta maendeleo ya taifa huku akitolea mfano katika sekta ya elimu ambayo alidai miaka50 ya uhuru bado mwanafunzi wa Tanzania anakaa chini huku tukingojea msaada toka kwa wafadhili ndio watoe fedha za madawati.

Baada ya hotuba hiyo ikafika kwa wakati wa kuwaalika wageni kwa ajili ya kuchangia ujenzi wa taasisi ya saratani ya Bishop Moshi huku wa kwanza akiwa ni Mbunge wa Jimbo la Vunjo ,Dkt Mrema ambaye alifika mbele na kupeana mkono na baba askofu kisha akamwita mkewe Rose Mrema na kutoa kiasi cha sh laki tano.

Aliyefuatia alikuwa ni Mbunge Mbatia ambaye kabla ya kuchangia alianza kwa kusema kuwa yeye katika maswala ya elimu yeye amekwisha toa kiasi cha sh Milioni 10 kwa ajili ya shule ya sekondari ya kumbukumbu Stephano Moshi huku akihadi kutoa kiasi cha sh mil 2 kwa ajili ya taasisi hiyo hali iliyozua shangwe kubwa toka kwa waumini.

Hali hiyo ilionekana kumvuruga Mrema ambaye alilazimika kumoba msaidizi wa askofu kupatiwa nafasi ya kuzungumza kwa kuwa yeye ndiye mbunge mwenyeji ambapo alipewa na kuanza kuzungumzia maswala ya mahakama ya kadhi hali iliyozua minong'ono miongoni mwa waumini.

baadae Mrema alionekana kutoka nje huku akisindikizwa na mkewe na baadae alielekea kwenye gari lake kabla ya kumalizika kwa shughuli za ibada hiyo na kuamua kuondoka kwa kile kilichodaiwa kutojisikia vizuri.

wakati shughuli za ibada hiyo zikiendelea Mbatia alipata nafasi ya kutia saini kitabu cha kumbukumbu ya Akofu Moshi na baadae kuweka shada la maua katika kaburi la marehemu Moshi.

wakiwa katika eneo la chakula ,baba askofu Dkt Shoo alimkabidhi ,mbatia Ndafu huku akisema kuwa wameamua kukabidhi chakula hicho ili kumpa nguvu katika mapambano yake katika kusaidia maendeleo ya nchi hususani katika swala la elimu.

Mwanza in perspective


Monday, May 11, 2015

Mkutano wa Bunge, Ratiba


JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
BUNGE LA TANZANIA

TAARIFA KWA UMMA
YAH: MKUTANO WA ISHIRINI WA BUNGE LA KUMI KUANZA DODOMA TAHERE 12 MEI 2015
_______________


1.0       UTANGULIZI
Mkutano wa Ishirini (20) wa Bunge la Kumi (10) unatarajia kuanza mjini Dodoma tarehe 12 Mei 2015. Mkutano huo ambao ni mahususi kwa ajili ya kujadili na kupitisha Bajeti ya Serikali ndiyo utakaokuwa mkutano wa mwisho wa Bunge hili kabla ya kuvunjwa na baadaye kufanyika Uchaguzi Mkuu mwezi Oktoba 2015.

Hivyo, Wabunge wote wanapaswa kuwa wamewasili mjini Dodoma  ifikapo Jumapili tarehe 10 Mei 2015 tayari kuhudhuria kikao cha briefing siku  ya Jumatatu tarehe 11 Mei, 2015.

2.0       SHUGHULI ZITAKAZOTEKELEZWA
Katika Mkutano huu kutakuwa na wastani wa maswali 295 ya msingi yatakayoulizwa na kupatiwa majibu. Aidha, kutakuwa na wastani wa maswali 56 atayoulizwa Waziri Mkuu na kuyapatia majibu kwa mujibu wa Kanuni ya 38(1) ya  Kanuni za Kudumu za Bunge Toleo la Aprili 2013.

Aidha, katika mkutano huo, taarifa ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) ya mwaka 2013/2014 itawekwa mezani na kufuatiwa na taarifa yenye majibu kuhusu hoja zilizotolewa na Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) kwa Hesabu za mwaka wa Fedha wa 2013/2014.

Baada ya hayo, Bunge litapokea na kujadili utekelezaji wa Wizara zote 24 wa Bajeti kwa mwaka wa Fedha unaoisha pamoja na Makadirio na Matumizi ya Serikali kwa mwaka wa Fedha 2015/2016.

Siku ya Alhamisi tarehe 11/Juni/2015 saa 4:00 (nne)  asubuhi Waziri anayehusika na Mipango atawasilisha taarifa ya Hali ya Uchumi wa Nchi, ikifuatiwa na hotuba ya Bajeti ya Serikali kwa mwaka wa fedha 2015/2016 itakayosomwa na Waziri wa Fedha saa 10:00 jioni. Wabunge wote mnaombwa kuwepo Dodoma.

Mjadala wa hotuba ya Bajeti ya Serikali kwa mwaka wa Fedha wa 2015/2016 utaanza na utafuatiwa na kupitishwa kwa Muswada wa Sheria ya Matumizi wa Mwaka 2015 pamoja na kujadili na kupitisha Muswada wa Sheria wa Fedha wa Mwaka 2015.

3.0 SHUGHULI NYINGINE
Shughuli za Mkutano wa 20 zinatarajiwa kumalizika tarehe 27 Juni, 2015 na kuhitimishwa kwa hotuba ya Waziri Mkuu ya kuliahirisha Bunge.

Ratiba kamili ya shughuli za Mkutano wa Ishirini wa Bunge la Kumi itapatikana kwenye Tovuti ya Bunge ambayo ni www.parliament.go.tz

Imetolewa na:
Ofisi ya Bunge,
Idara ya Habari, Elimu kwa Umma na Uhusiano wa Kimataifa,
DAR ES SALAAM
08  Mei 2015

RATIBA YA MKUTANO WA BUNGE LA BAJETI, KWA MWAKA WA FEDHA 2015/2016 TAREHE 12 MEI, 2015 HADI
27 JUNI, 2015

NA.
TAREHE NA SIKU

SHUGHULI HUSIKA NA WIZARA
1.
JUMAMOSI
na
JUMAPILI
09/05/2015 -10/05/2015
Wabunge kuelekea Dodoma kutoka Dar es Salaam na sehemu mbalimbali.
2.
JUMATATU
11/05/2015

Saa 4.00 Asubuhi


Saa 10.00 Jioni


·    Kikao cha Pamoja cha Kamati ya Uongozi na Kamati ya Bajeti (Ukumbi wa Pius Msekwa)

·    Kikao cha Briefing kwa Wabunge wote
(Ukumbi wa Pius Msekwa)
3.
JUMANNE - JUMAMOSI
12/5/2015 - 16/5/2015
Mkutano wa Bunge kuanza kwa shughuli zifuatazo.

(i)          Maswali ;

HOTUBA YA BAJETI YA OFISI YA WAZIRI MKUU: (Siku 5)
·      SERA, URATIBU NA BUNGE.

·      UWEKEZAJI NA UWEZESHAJI.

·      TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA
4.
JUMATATU
18/5/2015
  • Maswali

HOTUBA YA BAJETI YA OFISI YA RAIS:

  • MENEJIMENTI YA UTUMISHI WA UMMA

  • UTAWALA BORA

  • MAHUSIANO NA URATIBU

5.
JUMANNE
19/5/2015

  • Maswali

HOTUBA YA BAJETI YA OFISI YA MAKAMU WA RAIS (MUUNGANO NA MAZINGIRA).
6.
JUMATANO
20/5/2015
  • Maswali

  • HOTUBA YA BAJETI YA WIZARA KILIMO, CHAKULA NA USHIRIKA

7.

ALHAMISI
21/5/2015
  • Maswali

  • HOTUBA YA BAJETI YA WIZARA KATIBA NA SHERIA
8.
IJUMAA
22/5/2015


·    Maswali

·    HOTUBA YA BAJETI YA WIZARA YA MAMBO YA NDANI YA NCHI

·    HOTUBA YA BAJETI YA WIZARA YA ULINZI NA JESHI LA KUJENGA TAIFA.
9.
JUMAMOSI
23/5/2015
  • HOTUBA YA BAJETI YA WIZARA YA MIFUGO NA UVUVI
10.

JUMATATU
25/5/2015
·    Maswali

·  HOTUBA YA BAJETI YA WIZARA YA MAENDELEO YA JAMII, JINSIA NA WATOTO

·    HOTUBA YA BAJETI YA WIZARA YA KAZI NA AJIRA.
11.
JUMANNE
26/5/2015
  • Maswali

·    HOTUBA YA BAJETI YA WIZARA YA VIWANDA NA BIASHARA

·    HOTUBA YA BAJETI YA WIZARA YA MAWASILIANO, SAYANSI NA TEKNOLOJIA
12.
JUMATANO
27/5/2015
·    Maswali

·    HOTUBA YA BAJETI YA WIZARA YA UJENZI
13.
ALHAMISI
28/5/2015
·    Maswali

  • HOTUBA YA BAJETI YA WIZARA YA MALIASILI NA UTALII.

·    HOTUBA YA BAJETI YA WIZARA YA HABARI, VIJANA, UTAMADUNI NA MICHEZO

14.
IJUMAA
29/5/2015
·    Maswali

·    HOTUBA YA BAJETI YA WIZARA YA USHIRIKIANO WA AFRIKA MASHARIKI.

·    HOTUBA YA BAJETI YA WIZARA YA MAMBO YA NJE NA USHIRIKIANO WA KIMATAIFA.
15.
JUMAMOSI
30/5/2015
·    HOTUBA YA BAJETI YA WIZARA YA UCHUKUZI
16.
JUMATATU
 01/6/2015
  • Maswali

  • HOTUBA YA BAJETI YA WIZARA YA ELIMU NA MAFUNZO YA UFUNDI
17.
JUMANNE
02/6/2015


·    Maswali

·    HOTUBA YA WIZARA YA AFYA NA USTAWI WA JAMII
18.
JUMATANO
03/6/2015
·    Maswali

  • HOTUBA YA BAJETI YA WIZARA YA MAJI.
19.
ALHAMISI
04/6/2015

·    Maswali

·    HOTUBA YA BAJETI YA WIZARA YA ARDHI, NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI
20.
IJUMAA
05/6/2015
·    Maswali.

·    HOTUBA YA BAJETI YA WIZARA YA NISHATI NA MADINI.
21
JUMAMOSI
06/06/2015
  • HOTUBA YA BAJETI YA WIZARA YA FEDHA
22.
          JUMATATU  - JUMATANO
08/6/2015 – 10/6/2015
  • Maswali;

Serikali  kushauriana na Kamati ya Bajeti Kufanya Majumuisho kuzingatia Hoja zenye Maslahi kwa Taifa zilizojitokeza wakati wa kujadili Bajeti za Wizara;(Siku 3)
23.
ALHAMISI
11/6/2015
·         Maswali

(i)             Waziri anayehusika na Mipango Kusoma Taarifa ya Hali ya Uchumi.

(ii)           Waziri wa Fedha Kusoma Hotuba ya Bajeti ya Serikali.

24.
IJUMAA
12/6/2015
Wajumbe Kusoma na kutafakari Hotuba ya Bajeti.
25.
JUMATATU - JUMANNE
15/6/2015 - 23/6/2015


·      Maswali

·      MJADALA KUHUSU BAJETI  YA SERIKALI
(Siku 7)
26.
JUMATANO
24/6/2015
·    Maswali

·    Muswada wa Sheria ya Fedha za Matumizi (The Appropriation Bill, 2015)
·    Muswada wa Sheria ya Fedha (The Finance Bill, 2015)
27.
ALHAMISI - IJUMAA
25/6 – 26/6/2015

·    Maswali
·    Muswada wa Sheria ya Fedha (The Finance Bill, 2015)
28.
JUMAMOSI
27/6/2015

             KUFUNGA BUNGE