.

.
.

.

.
.

.

.
.

.

.
.

.

.
.

.

.
.

.

.
.

Thursday, June 30, 2011

HABARI NJEMA KWA WANAOJENGA DAR ES SALAAM


Ubora wake unazidi matarajio


Usafiri upo


Utaratibu wa malipo unazungumzika


Viwango vya hali juu

Wednesday, June 29, 2011

Spika Makinda Uso kwa uso na Askofu Mkuu Mokiwa





       Askofu Mkuu wa Anglican Dkt Valentino Mokiwa (kulia) akimpokea na kumkaribisha Spika wa Bunge la Tanzania Mhe. Anne Makinda mara alipowasili katika ofisi za Christian Council of Tanzania (CCT) mjini Dodoma leo. Spika Makinda yuko kwenye mchakato wa kukutana na vyama vyote vya siasa, taasisi za dini, makundi ya wanaharakati, NGOs, Shirikisho la wanafunzi wa Elimu ya Juu, Wasomi na Vyombo vya Habari ili kupata muafaka wa kuunda chombo kitakachoratibu maoni ya wananchi juu ya uundwaji wa Katiba mpya.

Mwenyekiti wa CCT  Askofu Dkt. Peter Kitula akitoa utambulisho na utanguli wa mwenendo wa majadiliano katika mkutano huo.

     Askofu Mkuu Dkt Walentiono Mokiwa (kushoto) akitoa mchango wake. Kulia ni Mchungaji Dkt. Leonard Mtaita


       Spika Makinda (kulia) na Mwenyekiti wa Kamati ya Katiba ,Sheria na Utawala Mhe. Pindi Chana wakifuatilia kwa makini mjadala huo.

Askofu Mkuu Mokiwa akikemea upotoshwaji wowote utakaojitokeza wakati wa machakato wa katiba mpya

  
 Picha ya pamoja ya viongozi hao wa Dini na Mhe. Spika















Tuesday, June 28, 2011

Bunge lapokea kombe la ushindi Utumishi wa Umma 2011

Cheti maalumu cha ushiriki na ushindi wa Ofisi ya Bunge katika maadhimisho ya Utumishi wa Umma 2011


Spika wa Bunge Mhe. Anne Makinda akipokea Kikombe cha Ushindi kutoka kwa Kaimu Katibu wa Bunge Bw. John Joel
 (kushoto) na kukionyesha rasmi kwa Bunge zima leo




Hongera kwa watumishi waliofanikisha: Spika Makinda

Monday, June 27, 2011

Uwapo Dodoma unakula wapi?...... Cipe Cito !

Mama Cipe (blaus nyekundu) na Maafisa wa Bunge wakijichana kwenye mgahawa maarufu wa Cipe uliko kando kidogo ya Club maarufu ya 84

Ukiwa Cipe unapata aina zote za vyakula vya kienyeji na kigeni

Makange, Punjap, Sato, Sangara, Kibakwe, Michemsho aina zote, ushindwe mwenyewe

Uwapo Cipe jisikie nyumbani.............

Ugeni Bungeni Dodoma na Ziara ya Mama Obama Afrika Kusini

Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Mizengo Pinda akibadilishana
mawazo na Spika wa bunge Mhe Anne Makinda kwenye viwanja vya Bunge jana

Wageni kutoka Vietnam wakiwa kwenye picha ya pamoja na Mhe. Spika
Spika Makinda akiongoza kikao na wageni kutoka Vietnam

Balozi wa Vietnam nchini Tanzania Mhe. Nguyen akiwatambulisha wageni hao


Mke wa Rais wa Marekeni Bi Mchelle Obama pamaja na watoto wake wakimfurahi Mzee Nelson Mandela walipomtembelea nyumbani kwake Jo'burg hivi karibuni


Mzee Mandela na Mama Obama wakifuatilia kitabu cha maisha yake.

Mama Obama na Mama Graca Machel Mandela


Bi Michelle Obama na Mke wa Rais wa Afrika Kusini Bi.Nompumelelo Ntuli-Zuma

Bi Michelle Obama akiwahutubia wanawake vijana wa Afrika Kusini katika Ukumbi wa kanisa la Regina Mundi

Wanawake vijana wakiwa na Bi Obama kwenye maeneo ya kihistoria ya Afrika Kusini

Bi Obama akiukumbatia umati mkubwa wa vijana

Bi obama akifurahia jambo na watoto

Ngoma ya ukaribisho kwa Bi Michelle Obama



Mke wa rais wa Marekani akipanda mboga aina ya spinachi

Mama Obama akidhihirisha umaarufu wake wa kucheza kiduku

Friday, June 24, 2011

Bunge latwaa Kombe Utumishi wa Umma

Picha zote: Maafisa wa Ofisi ya Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wakishangilia baada ya banda la Ofisi ya Bunge kukabidhiwa Kombe la mshindi wa pili katika medani ya maelezo na ufafanuzi  kwenye kilele cha maadhimisho ya Utumishi wa Umma tarehe 23 Juni 2011. Washiriki katika maadhimisho hayo kutoka ndani na nje yaTanzania walikuwa 185  na yalidhaminiwa na Umoja wa mataifa na Umoja wa Africa.