.

.
.

.

.
.

.

.
.

.

.
.

.

.
.

.

.
.

.

.
.

Tuesday, November 4, 2014

Msaada tutani.

Ben Komba/Pwani.

Mtoto wa kike BI.ELIZABETH SAMUEL mwenye umri wa miaka 13 mkazi wa Mailimoja shule amepotea katika mazingira ya kutatanisha takriban wiki moja,mjini Kibaha mkoa wa Pwani.

Mjomba wa mtoto ELIZABETH, BW.BONIFACE KITILA amesema siku aliyopotea alikuwa amevaa sketi ya bluu ya shule na fulana ya rangi ya ugoro iliyokuwa na maandishi ya LOVE  maeneo ya tumboni akiwa bila viatu.

Bw.KITILA ameongeza kuwa mtoto huyo ambaye ni mgeni mjini Kibaha, ametokea Singida kwa lengo la kuja kuishi na shangazi yake mjini Kibaha na mpaka sasa juhudi mbalimbali zimeshafanyika ikiwa pamoja na kuripoti kituo cha Polisi.

Ametoa wito kwa wananchi kutoa taarifa kituo chochote cha Polisi watakapomuona mtoto anayefanana na na wasifa uliotolewa,au apigiwe simu namba 0765871647.