.

.
.

.

.
.

.

.
.

.

.
.

.

.
.

.

.
.

.

.
.

Tuesday, November 4, 2014

Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete amemtumia Salamu za Rambirambi Katibu Mkuu wa Umoja wa Vijana wa CCM (UVCCM) Taifa, Bwana Sixtus Mapunda kuomboleza kifo cha Katibu wa UVCCM.




THE UNITED REPUBLIC OF TANZANIA
DIRECTORATE OF PRESIDENTIAL COMMUNICATIONS

Telephone: 255-22-2114512, 2116898
Website : www.ikulu.go.tz              

Fax: 255-22-2113425



PRESIDENT’S OFFICE,
      STATE HOUSE,
              1 BARACK OBAMA ROAD,  
11400 DAR ES SALAAM.
Tanzania.
 

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Taifa, Mheshimiwa Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete amemtumia Salamu za Rambirambi Katibu Mkuu wa Umoja wa Vijana wa CCM (UVCCM) Taifa, Bwana Sixtus Mapunda kuomboleza kifo cha Katibu wa UVCCM Wilaya ya Arumeru, Lucy Bongele kilichotokea tarehe 2 Novemba, 2014 kwa ajali ya gari.

Ajali hiyo ilitokea katika Wilaya ya Ngorongoro baada ya gari walilokuwa wakisafiria aina ya Land Cruiser Prado Namba T380 ADP kuacha njia na kupinduka wakati Katibu huyo na Viongozi wenzake wa UVCCM walipokuwa wakienda kumsimika Bruno Kawasange kuwa Kamanda wa UVCCM Wilaya ya Ngorongoro.  Ajali hiyo iliwajeruhi viongozi wengine watano wa UVCCM pamoja na Dereva.

“Nimepokea kwa mshtuko na masikitiko makubwa taarifa ya kifo cha ghafla cha Katibu wa UVCCM Wilaya ya Arumeru, Lucy Bongele kilichosababishwa na ajali ya gari, wakati Katibu huyo alipokuwa akienda kumsimika Bruno Kawasange kuwa Kamanda wa UVCCM wa Wilaya ya Ngorongoro”, amesema Rais Kikwete katika Salamu zake.

“Kutokana na kifo cha hicho, ninakutumia Salamu za Rambirambi kutoka dhati ya moyo wangu kwa kumpoteza mmoja wa vijana hodari na wachapakazi katika safu ya uongozi ya UVCCM. Kuondoka kwake kumeacha pengo kubwa katika safu ya uongozi wa UVCCM  katika Wilaya ya Arumeru”, amesema Rais Kikwete.

“Naomba Mwenyezi Mungu, Mwingi wa Rehema aipokee na kuilaza mahala pema peponi Roho ya Marehemu Lucy Bongele. Namwomba Mola awawezesha kupona haraka majeruhi wote wa ajali hiyo  wapone haraka ili waendelee kusaidia UVCCM katika uongozi wake”, ameongeza kusema Rais Kikwete katika salamu zake.

Rais Kikwete amewaomba ndugu na jamaa wa Marehemu Lucy Bongele wawe wavumilivu na wenye subira wakati huu wanapoomboleza kifo cha mpendwa wao, na amewahakikishia kuwa yuko pamoja nao katika kipindi chote cha maombolezo.


Imetolewa na;
Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais,
Ikulu – Dar es Salaam.
4 Novemba,2014