.

.
.

.

.
.

.

.
.

.

.
.

.

.
.

.

.
.

.

.
.

Wednesday, April 2, 2014

Bunge la Afrika Mashariki lachafuka, laahirishwa


ARUSHA,Bunge la Afrika Mashariki (Eala) limeanza kuonekana kufanana na Bunge la Katiba linaloendelea mjini Dodoma.
Bunge hilo jana limevunjika bila kujulikana litakutana tena lini baada ya kuibuka mabishano ya kisheria kuhusu hoja ya kutokuwa na imani na Spika, Margret Zziwa.
Hoja ya kumng’oa Spika Zziwa ilianza kuzungumzwa kwenye vyombo vya habari vya Afrika Mashariki kwa wiki kadhaa sasa na hatimaye kuwasilishwa jana na Mbunge Peter Mathuki kutoka Kenya kwa niaba ya wenzake Shy-Rose Bhanji wa Tanzania, Nyiranilimo Odette wa Rwanda na Hafsa Mossi kutoka Burundi.
Awali Bunge hilo linalopaswa kuanza vikao vyake saa 8:00 mchana lilichelewa kuanza hadi Saa 9:44 alasiri baada ya wabunge kugoma kuingia ukumbini walipobaini kuwa hoja ya kumng’oa Spika haikuwa miongoni mwa shughuli za Bunge kwenye kikao cha jana.
Baada ya mashauriano ya muda mrefu kati ya ofisi ya spika, Mwanasheria wa EAC, Wakili Wilbert Kaahwa na Katibu wa Bunge, Kenneth Madete, Spika Zziwa alikubali hoja ya kumng’oa iongezwe kwenye orodha ya shughuli za Bunge ndipo Mbunge Mathuki alipopewa fursa ya kuwasilisha hoja.
Hata hivyo dakika moja tangu Mathuki alipoanza kusoma maelezo ya hoja hiyo, Mbunge Fred Mukassa Mbidde aliinuka na kuomba mwongozo wa Spika na alipopewa nafasi, alipinga hoja hiyo kuwasilishwa na kujadiliwa kwa madai kuwa kuna kesi katika Mahakama ya Afrika Mashariki (EACJ) inayohusiana na hoja hiyo.
Akifafanua Mbidde alisema kesi hiyo inaomba mwongozo na ufafanuzi wa kisheria kuhusu kanuni ya 9 ya Bunge la EAC inayoelekeza utaratibu wa kumwondoa madarakani Spika wa Eala iwapo kutatokea haja ya kufanya hivyo.
Wakati Mbunge Mbidde akiwa bado amesimama huku akiendelea kutoa hoja yake, Mbunge Joseph Ombasa kutoka Kenya aliinuka na kumpinga mbunge mwenzake akisema anataka kulipotosha Bunge kwani kifungu 38 (3) kinaruhusu Bunge hilo kujadili hoja yoyote yenye masilahi ya umma wa EAC ikiwamo hilo la kumng’oa Spika.
Baada ya hoja ya Ombassa, Mwanasheria wa EAC, Kaahwa alisimama kutoa ufafanuzi wa kisheria licha ya kukiri kuwapo kesi mahakamani alisema tayari mahakama hiyo imetoa uamuzi mdogo kuwa shauri hilo haliwezi kuzuia shughuli na mjadala wowote wenye nia ya kumwondoa Spika madarakani
Hoja hiyo ya Mwanasheria ilimwibua tena Mbunge Mbidde aliyehoji kwanini maelezo na ufafanuzi wa mwanasheria huyo yanatoa mwelekeo wa ulipo msimamo wake kuhusu hoja iliyokuwa mbele ya Bunge.
Katika hali iliyoashiria uwapo wa kimkakati kati ya kiti cha Spika na Mbunge Mbidde, Spika Zziwa naye aliunga mkono hoja ya mwanasheria kuonekana anaelemea upande unaotaka ang’olewe.
Kauli hiyo ilimwamsha kitini Mwanasheria Kaahwa aliyemhakikishia Spika kuwa hoja yake inalenga kusaidia uendeshaji bora wa Bunge na siyo kuegemea upande unaotaka kumng’oa.MWANANCHI










Chini ni saini za wabunge za kumwengua Spika