.

.
.

.

.
.

.

.
.

.

.
.

.

.
.

.

.
.

.

.
.

Wednesday, March 26, 2014

Ikulu yatoa Rambimbi Kifo cha RC Tupa


THE UNITED REPUBLIC OF TANZANIA
DIRECTORATE OF PRESIDENTIAL COMMUNICATIONS

Telephone: 255-22-2114512, 2116898
              press@ikulu.go.tz             

Fax: 255-22-2113425



PRESIDENT’S OFFICE,
      THE STATE HOUSE,
              P.O. BOX 9120,  
DAR ES SALAAM.
Tanzania.
 
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

SALAMU ZA RAMBIRAMBI ZA RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA, MHESHIMIWA DKT. JAKAYA MRISHO KIKWETE

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete amemtumia Salamu za Rambirambi Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa  na Serikali za Mitaa (TAMISEMI)  Mhe. Hawa A. Ghasia kufuatia kifo cha Mkuu wa Mkoa wa Mara, Mhe. John Gabriel Tuppa, aliyefariki leo tarehe 25 Machi, 2014 katika Hospitali ya Wilaya ya Tarime.

Pokea rambirambi zangu za dhati na  masikitiko makubwa kufuatia   kifo cha Mhe. John Gabriel Tuppa. Ni huzuni kubwa na pigo kwa Serikali na hasa kwa Watendaji wenzake mkoani Mara ambao alikuwa akifanya nao kazi.    Marehemu John Gabriel Tuppa amefariki leo tarehe 25 Machi,2014 katika Hospitali ya Wilaya ya Tarime.

Rais pia amemwomba Mhe. Ghasia amfikishie salamu za pole kwa Mke  wa Marehemu,Watoto na Familia ya Marehemu kwa kuondokewa na kipenzi chao. Rais amesema, anaelewa machungu wanayoyapitia katika kipindi hiki kigumu kwani wamepoteza nguzo imara waliyokuwa wakiitegemea katika maisha yao.

“Hakika tumempoteza kiongozi mchapakazi ambaye amekuwa akijituma  na kuwatumikia Wananchi wake hadi dakika za mwisho za uhai wake.  Pengo aliloliacha Marehemu Tupa haliwezi kuzibika kamwe lakini hatuna budi kumwombea kwa Mwenyezi Mungu kuipumzisha roho ya Marehemu mahali pema peponi” Amina.

Taratibu na maandalizi ya mazishi zinafanywa kwa ushirikiano wa Familia, Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mara na Ofisi ya Waziri Mkuu TAMISEMI.

Marehemu Tupa alizaliwa tarehe 01 Januari, 1950 na katika enzi za uhai wake amewahi kuongoza Wilaya za  Chunya, Mwanga, Bukoba, Muleba na Dodoma kabla ya kuteuliwa kuwa Mkuu wa Mkoa wa Mara Mwaka 2011. Ameacha Mke na watoto watano.

  
Mwisho!

Imetolewa na;

Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais,
Ikulu,
DAR ES SALAAM.

25 Machi,2014