.

.
.

.

.
.

.

.
.

.

.
.

.

.
.

.

.
.

.

.
.

Sunday, September 25, 2011

Wananchi wa Njombe walivyojiandaa kuwa mkoa mpya


Kilimo cha Chai Njombe

Mkoa mpya wa Njombe umejiandaaje? (Na Prosper Minja)
Jamii maskini kwa kawaida huwa na vipaumbele vingi. Matokeo yake ni kushindwa kuvitekeleza. Wananchi wa mkoa mpya wa Njombe ambao ni wachapa kazi kweli kweli wameikataa falsafa hiyo na wamejiwekea vipaumbele vichache na vya uhakika ili kuujenga mkoa wao. Vipaumbe vya wananjombe ni:
1.       Elimu- Kwa kujitolea wananchi wa vijiji na kata za Katulila, Madobole, Miva, Lusitu, Mtila, Mbega, Matola, Luponde, Itulike, Ramadhani, Kihesa, Utalingolo, Ihalula, Nolle, Mamongoro, Makowo, Ng’elamo, Yakobi, Igominyi, Idunda, Idihani, Lugenge na Kiyaula wameamua kujikita katika suala zima la elimu kwa shule za awali, msingi na sekondari.  Majenfo mzuri ya ya kisasa yako katika hatua mbali mbali. Ombi lao ni waalimu wa kutosha.

2.       Afya: Ili kuimarisha afya wananchi hao wako katika mpango wa kuwa na zahanati katika kila kata. Tayari kwa kujitolea wameanza ujenzi wa zahanati hizo. Ombi lao ni kupatiwa wauguzi wa kutosha.


3.       Kilimo: kutokana na hali ya hewa nzuri ya nyanda za juu kusini, wananjombe hawa wamejizatiti katika kilimo cha chai, mahindi, viazi mviringo na misitu ya mbao.

4.       Miundombinu:  kwa sehemu kubwa wananjombe wamejitahidi sana kutengeneza barabara za ndani na wanaamini ni kwa barabara nzuri wataweza kufaidika na  fursa zitokanazo na migodi ya machimbo ya chuma na mkaa wa mawe ya Mchuchuma na Liganga


Jengo la SACOSS Kata ya Utalingolo


Wananjombe kwenye mkutano wa Hadhara

Kituo cha Afya - Ihalula (Ujenzi upo katika hatua za mwisho)

Misitu ya Mbao - Njombe

Ujenzi wa Zahanati kijiji cha Nolle

Mbunge wa Njombe Kusini Mhe. Anne Makinda akiweke jiwe la msingi katika Zahanati ya kijiji cha Utalingolo

Ujenzi na ukarabati wa shule ya msingi Mbega

ujenzi wa zahanati

Ujenzi wa mabweni ya wanafunzi wa shule za sekondari (ufadhili wa kampuni ya Chai)

Wananchi wenye ari ya kujenga mkoa wao

Majengo ya Zamani- kumbukumbu za walikotoka wananjombe

Usanifu mpya wa majengo

Wananchi wakipata elimu ya Bunge kwa njia ya vipeperushi

Vijana wa Njombe kusini wakimsikiliza na kumuuliza maswali Mbunge wao katika kata ya Matola

wanafunzi wa sekondari ya matola wakiweka bayana mikakati yao ya masomo, huku Mbunge wao akiwasikiliza kwa makini

Kipaumbele ni elimu

Sura za kazi



Spika wa Mhe. Anne Makinda akikata utepe kuashiria ufunguzi wa nyumba ya mganga- Makowo

Wakati wa kusubiri madawati ya kisasa hakuna haja watoto kukaa chini - Ubunifu

Taifa la kesho- urithi pekee ni eleimu

Sekondari za kata mkoani Njombe-Hapa ni kitulila


Vyumba vya kupumzisha wagonjwa katika zahanati ya Miva- ujenzi unaendelea

Wanafunzi wenye ari na masomo


Muonekano wa mabweni ya wanafunzi

Ujenzi wa zahanati Mtila


Zahanati Mtila


Majengo ya Madara ya kisasa

Majengo ya shule ambayo sasa wananjombe wameamua kuachana nayo

Nyumba za waalimu


Jengo la ofisi ya waalimu -nguvu za wananchi


Hapa umeingia St Benedict Academy-Kipimo cha ukakamavu


St  Benedict

Kihesa


Wananchi wa Kihesa wakimsiliza Mbunge wao wa Njombe Kusini

Taswira ya mkoa mpya wa Njombe

Watoto wa shule ya awali wakitoa ujumbe wa UKIMWI kwa Spika wa Bunge


Mhe. Makinda akiweka jiwe la msingi katika zahanati ya Kiyaula