.

.
.

.

.
.

.

.
.

.

.
.

.

.
.

.

.
.

.

.
.

Wednesday, June 29, 2011

Spika Makinda Uso kwa uso na Askofu Mkuu Mokiwa





       Askofu Mkuu wa Anglican Dkt Valentino Mokiwa (kulia) akimpokea na kumkaribisha Spika wa Bunge la Tanzania Mhe. Anne Makinda mara alipowasili katika ofisi za Christian Council of Tanzania (CCT) mjini Dodoma leo. Spika Makinda yuko kwenye mchakato wa kukutana na vyama vyote vya siasa, taasisi za dini, makundi ya wanaharakati, NGOs, Shirikisho la wanafunzi wa Elimu ya Juu, Wasomi na Vyombo vya Habari ili kupata muafaka wa kuunda chombo kitakachoratibu maoni ya wananchi juu ya uundwaji wa Katiba mpya.

Mwenyekiti wa CCT  Askofu Dkt. Peter Kitula akitoa utambulisho na utanguli wa mwenendo wa majadiliano katika mkutano huo.

     Askofu Mkuu Dkt Walentiono Mokiwa (kushoto) akitoa mchango wake. Kulia ni Mchungaji Dkt. Leonard Mtaita


       Spika Makinda (kulia) na Mwenyekiti wa Kamati ya Katiba ,Sheria na Utawala Mhe. Pindi Chana wakifuatilia kwa makini mjadala huo.

Askofu Mkuu Mokiwa akikemea upotoshwaji wowote utakaojitokeza wakati wa machakato wa katiba mpya

  
 Picha ya pamoja ya viongozi hao wa Dini na Mhe. Spika