.

.
.

.

.
.

.

.
.

.

.
.

.

.
.

.

.
.

.

.
.

Sunday, June 7, 2015

UNDP yafurahishwa na Bunge

Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP) kupitia mradi wake wa kuwawezesha Wabunge (LSP) hivi karibuni limemkabidhi Spika wa Bunge Mhe. Anne Semamba Makinda (kwa niaba ya Ofisi ya Bunge) gari aina ya Land Cruiser V8 baada ya kuridhishwa na utaratibu mzuri wa Ofisi ya Bunge katika kuusimamia mradi huo. Gari hilo lenye thamani ya shilingi milioni 96 litatumika katika miradi ya kuwajengea uwezo waheshimiwa wabunge pamoja na watumishi wa Ofisi ya Bunge. Makabidhiano hayo yalifanyka katika Ofisi ya Bunge mjini Dodoma mbele ya Makamishna wa Bunge pamoja na Maafisa wa ngazi za juu wa Ofisi ya Bunge.