Kukata utepe..... Mmiliki Bwana Kapande (shati jeupe) nyuma yake ni mkewe ambaye ndiye msukumo mkubwa.... kutoka kushoto ni Meya wa Trollhattan, Paul Akerlund na Balozi wa Tanzania nchini Sweden Mhe. Dora Msechu
Katika kazi yake ya
upishi, amebahatika kuwapikia watu mashuhuri duniani, baadhi wakiwa Andrew
Young, Mchungaji Jesse Jackson, Robert Mugabe (Rais wa Zimbabwe), Paul Kagame
(Rais wa Rwanda), Benjamini Mkapa (Rais mstaafu wa Tanzania), Raila Odinga
(Waziri Mkuu wa zamani wa Kenya), Daniel Arap Moi (Rais Mstaafu wa Kenya),
Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani Bi. Hillary Clinton na mumewe Bill
Clinton, Mke wa Rais wa zamani wa Marekani Laura Bush.
Wengine ni Rais wa
Zanzibar Dk. Ali Mohamed Shein, mwigizaji Chris Tucker, Rais wa zamani wa
Afrika Kusini hayati Mzee Nelson Mandela, Koffie Olomide, Youssour ndour,
Arsene Wenger (Kocha wa Arsenal ya England), Gianluca Vialli (nyota wa zamani
wa Italia aliyewahi kuichezea na kuinoa Chelsea ya England), Rais wa Congo DRC,
Joseph Kabila, Billy Gates na wengine wengi.
|